Mambo 15 aliyoyaongea Diamond Platnumz leo kwenye kipindi cha Clouds360 cha Cloudsfm

Kuingia Kwenye Droo Yetu Ya Wasafi WCB Daily, Bonyeza Mshale kama huu

                                             dinsta
Jumanne ya March 14, 2017 kupitia #Clouds360 ya Clouds TV, staa wa BongoflevaNaseeb Abdul a.k.a Diamond Platinumz amefanya interview na kueleza mambo mengi kuhusu muziki wa Tanzania, serikali kusaidia sanaa, Rais kuweka mkono wake kwenye muziki, wasanii kulipa kodi, kutangaza utalii na kipi kinaendelea kati yake na staa mwenzake Alikiba.
Nimekukusanyia hapa mambo 15 ameyaongea leo Diamond Platnumz.



Naomba serikali iwasaidie vijana wa vibanda vya chipsi pamoja na bodaboda ishu ya muda wa saa sita wapewe ulinzi 




Namuomba Rais Magufuli kama anavyosaidia mengine kwa haraka na kwenye sanaa weka mkono wako baba tunakutegemea 



View image on TwitterView image on Twitter

Tumeshirikiana na Joseph Kusaga kuaanda product ya Chibu Perfume, tutazindua bidhaa hii fahari ya Tanzania 



Hili suala la Serengeti Boys ni jukumu letu kulibeba kama Taifa tuunganishe nguvu ushindi wetu ushindi wao 



Nilikutana na  Nairobi tukazungumza, maneno yanasemwa na watu wa katikati baadhi ya media zinachochea tu 



Tulilipa Kodi ya TRA milioni 35 ni uthubutu tunaweza kulipa kodi nyingi, serikali inabidi itulinde kwenye sanaa 



Watu walizungumza vibaya mimi kupewa BenderΓ  ilisaidia sana kulitangaza taifa letu, nilimuomba Nape samahani 



Kipindi tunamuaga Rais Kikwete nilipata nafasi ya kuzungumza na Rais Magufuli nilimuomba tupate ukumbi wa kisasa 



Mimi ni kielelezo ndani na nje ya nchi watu wengi wameifahamu tanzania kupitia sanaa yetu lazima tujijenge 



Tangu mwezi wa 7 mpaka sasa sijapokea mauzo yangu nimeyasusa, kinachofuata itakuwa ni hatua za kimahakama 



Makonda ni mlezi wa WCB kila mwanadamu ana mapungufu yake tuangalie pia mazuri, ameonesha uthubutu kwenye kazi 



Msanii akihusishwa kwenye sakata la dawa za kulevya ni kuharibu brand, Serikali itumie busara kuzilinda na kesi. 



View image on TwitterView image on Twitter

Nilishawahi kwenda TANAPA kuomba niwe balozi wa utalii nitangaze nchi yangu lakini walitaka nijitolee bure tu. 



Tumeanzisha mtandao wetu wa kuuza na kusambaza nyimbo za wasanii online tumeongea na mashabiki watuunge mkono 




Watu wanashangaa mimi kutangaza vivutio vya Afrika Kusini sio kwamba nimekosa uzalendo, wameniona kupitia sanaa  
DOWLOAD APP YETU YA WCB DAILY HAPA CHINI

0 Response to "Mambo 15 aliyoyaongea Diamond Platnumz leo kwenye kipindi cha Clouds360 cha Cloudsfm"

Post a Comment